Storm FM

Costantine Morandi aomba mitano tena kwa wakazi wa Samina

9 October 2025, 5:34 am

Mgombea udiwani kata ya Mtakuja (CCM) Costantine Morandi akizungumza na wakazi wa Samina (hawapo pichani). Picha na Ester Mabula

Ikiwa zimesalia siku 19 tu kuweza kufanyika uchaguzi mkuu kwa mwaka 2025, wagombea wa nafasi mbalimbali wameendelea kunadi sera pamoja na ilani za vyama vyao.

Na: Ester Mabula

Mgombea udiwani katika kata ya Mtakuja kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi ambaye pia ni Meya mstaafu wa manispaa ya Geita Mhe. Costantine Morandi Oktoba 08, 2025 ameendeleza kampeni za kunadi sera zake na ilani ya chama chake sambamba na kuomba ridhaa ya wananchi kumchagua tena katika nafasi hiyo kwa awamu nyingine.

Akizungumza katika mkutano uliofanyika eneo la Samina Senta katika kata hiyo ameeleza vipaumbele vyake kuwa ni sekta za maji, elimu sambamba na miundombinu hususani nishati ya umeme huku akitaja miradi ambayo ametekeleza kwa awamu inayokamilika chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan.

Mgombea udiwani kata ya Mtakuja Costantine Morandi akizungumza na wananchi (hawapo pichani). Picha na Ester Mabula

Amewasihi wananchi kuchagua viongozi wa CCM ili waweze kukamilisha malengo na mipango mizuri waliyoanzisha kwenye sekta mbalimbali huku lengo kubwa likiwa ni kuchochea maendeleo.

Sauti ya mgombea udiwani kata ya Mtakuja (CCM) Costantine Morandi
Wananchi waliojitokeza kwenye mkutano kusikiliza sera za mgombea udiwani kata ya Mtakuja. Picha na Ester Mabula
Wananchi waliojitokeza kwenye mkutano kusikiliza sera za mgombea udiwani kata ya Mtakuja. Picha na Ester Mabula