Storm FM

Wamiliki magari binafsi walalamikiwa kubeba abiria Nyankumbu

8 October 2025, 5:28 am

Shuhuli mbalimbali zikiendelea katika stendi ya Nyankumbu manispaa ya Geita. Picha na Kale Chongela

“Suala hili tumekuwa tukilikomesha lakini inaonekana bado linajirudia kutokana na baadhi ya mawakala kuendelea kukiuka taratibu” – Mwenyekiti wa stendi Nyankumbu

Na: Kale Chongela

Baadhi ya wamiliki wa magari ya abiria katika kituo kidogo cha magari ya abiria kilichopo kata ya Nyankumbu, halmashauri ya manispaa ya Geita wamewalalamikia baadhi ya mawakala wanaotafuta abiria na kuwaelekeza kupanda magari binafisi ili hali magari hayo hayana leseni ya usafirishaji wa abiria.

Akizungumza na Storm FM jana Oktoba 07, 2025 kwa niaba ya  wamiliki wa magari ya abiria Shigogo Wiliam amesema jambo hilo linawakwamisha kwani wao hulipia leseni ya usafirishji wa abiria na kwamba jambo hilo linatakiwa kutatuliwa.

Sauti ya mmiliki wa gari la abiria Bw. Shigogo William

Baadhi ya mawakala ambao wamekuwa wakijihusisha na tabia hiyo ya  kutafuta abiria na kuwaelekeza kupanda gari binafisi wamepata nafasi ya kujibu tuhuma hizo zinazowakabili.

Sauti ya mawakala wa mabasi Nyankumbu
Viongozi wa stendi ya Nyankumbu manispaa ya Geita. Picha na Kale Chongela

Mwenyekiti wa stendi hiyo ya Nyankumbu Bw. Aloyce Kavula baada ya kupokea tuhuma hizo amesema amekuwa akijaribu kuzuia changamoto hiyo na kutoa adhabu kwa mawakala wanaokiuka lakini tabia hiyo imeendelea kujirudia.

Sauti ya mwenyekiti wa stendi ya Nyankumbu

Mwenyekiti wa umoja wa madereva wa magari ya abiria wa mkoa wa Geita amesema tabia hiyo inatakiwa kukoma mara moja na kwamba viongozi wa stendi wanatakiwa kuwajibika mara moja ilikukomesha changamoto hiyo

Sauti ya mwenyekiti wa madereva mkoa wa Geita
Kikao cha wamiliki wa mabasi na mawakala kilichoketi Oktoba 07, 2025. Picha na Kale Chongela