Storm FM

Wezi wabomoa na kuiba ndani ya duka Msalala road

5 September 2025, 11:32 am

Mmiliki wa duka akiangalia uharibifu wa miundombinu uliofanywa. Picha na Amon Mwakaobo

“Matukio ya vibaka na wezi kuiba katika mtaa huu yamekithiri hatuna amani, serikali iwashughulikie watu watakaobainika ili iwe fundisho” – Mwananchi

Na: Amon Mwakalobo

Watu wasiofahamika wanaosadikika kuwa ni wezi wamebomoa kibanda cha biashara (duka) cha Bw. Shemu Masato katika mtaa wa Msalala road, halmashauri ya manispaa ya Geita na kuiba vitu mbalimbali ikiwemo sukari na mafuta ya kupikia vyenye thamani ya shilingi laki nne.

Kwa mujibu wa mama mwenye nyumba Ester Mashiri alipopanga mfanyabiashara huyo na mfanyabiashara mwenyewe wanasimulia kusikitishwa na tukio hilo ambalo lilitokea majira ya saa kumi za Alfajiri ya Septemba 04, 2025.

Sauti ya mmiliki wa kibanda Bw. Shemu Masato
Sauti ya mwenye nyumba Bi. Ester Mashiri

Mmoja wa majirani wa nyumba hiyo ambaye Jenipher Justine amesema alisikia usiku mlango ukifunguliwa kwa kelele akapuuzia akifikiri ni majirani wanapigana.

Sauti ya jirani Bi. Jenipher Justine

Mama mwingine mpangaji wa nyumba hiyo ambaye ni Mtaalamu wa tiba asili Bi. Maisala Shaban amesema matukio ya wizi mtaani hapo yamezidi kwani wiki iliyopita tuu walivunja mlango wa chumba chake na kutaka kumuibia dawa zake za asili lakini hawakufanikiwa.

Sauti ya mpangaji aliyenusurika kuibiwa

Mlinzi wa eneo hilo akihojiwa na viongozi wa mtaa huo amesema aliacha lindo saa kumi za usiku pakiwa salama huku akiwa amefunga kamba na kwenda kulala.

Sauti ya mahojiano ya viongozi na mlinzi

Mwenyekiti wa serikali ya mtaa huo Bw. Sostenes Kalist amekiri kutokea kwa tukio hilo na kuwashauri wafanyabiashara kuhakikisha wanakuwa na walinzi wa kampuni na si mlinzi mmoja mmoja ambaye anapata wakati mgumu kulinda peke yake eneo kubwa.

Sauti ya mwenyekiti wa mtaa Sostenes Kalist