Storm FM

Picha: Mwenge wa uhuru wakabidhiwa Nyangh’wale

3 September 2025, 9:56 am

Makabidhiano ya mwenge wa uhuru yakifanyika kati ya DC Geita na DC Nyangh’wale. Picha na Kale Chongela

Ikumbukwe Mwenge wa uhuru ulipokelewa mkoani Geita Septemba mosi, 2025 ukitokea mkoani Mwanza ambapo umeendelea kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo.

Na: Kale Chongela

Mkuu wa wilaya ya Nyang’hwale  Mhe. Grace  Kigalame  ameupokea Mwenge wa Uhuru  kutoka kwa Mkuu wa wilaya ya Geita Hashim Komba

Makabidhiano yamefanyika asubuhi ya leo Septemba 03, 2025 katika viwanja  vya shule ya msingi Wavu katika kata ya Shabaka.

Mhe. Kigalame baadaya kuupokea Mwenge wa uhuru ametoa taarifa kuwa mwenge wa Uhuru ukiwa katika wilaya ya Nyang’hwale utakimbizwa kwa kilomita  58 na kutembelea jumla ya miradi 11 yenye thamani ya shilingi Bilioni 1.5

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ndugu Ismail Ally Ussi  amewataka wasimamizi wa miradi na wakuu wa idara kuhakikisha taarifa zote za mradi husika zinakuwepo kwenye mradi .