Storm FM

TAG yawakumbuka wajane na wahitaji Geita

20 August 2025, 9:00 pm

Baadhi ya wahitaji wakipokea msaada wa chakula kutoka katika kanisa la TAG. Picha na Kale Chongela

Jamii imetakiwa kuendelea kuwakumbuka wajane kwakuwa wengi wao wanapitia changamoto nyingi hususani za kiuchumi

Na Kale Chongela:

Kanisa la TAG Heri Wenye Moyo Safi Mtaa wa Nyantorotoro B Kata ya Nyankumbu Manispaa ya Geita limetoa msaada wa vyakula kwa watu wasiojiweza pamoja na wajane wanaoishi katika mtaa huo.

Akizungumza na Storm FM leo Agosti 18,2025 Mchungaji wa Kanisa hilo Eliya George amesema vyakula hivyo vimetokana na sadaka zinazotolewa na waumini pamoja na wananchi wanaounga mkono jitihada za kuendesha mikutano ya Injili za mitaa kwa mitaa.

Sauti ya Mchungaji
Baadhi ya wahitaji wakipokea msaada wa chakula kutoka katika kanisa la TAG. Picha na Kale Chongela

Baadhi ya wananchi waliopokea msaada huo wamesema wametiwa moyo na kitendo hicho cha kanisa, wakieleza kuwa kimewasaidia kukabiliana na changamoto za upungufu wa chakula majumbani mwao.

Sauti ya wanufaika wa msaada

Kwa upande wake, Balozi wa shina namba 20  Damiani Kagoma ameeleza kuwa msaada huo umeleta faraja kubwa katika jamii yake na kuonesha mfano wa mshikamano wa kijamii huku akisisitiza wananchi wa eneo hilo kuendeleza moyo wa kujitolea na kusaidiana.

Sauti ya Balozi wa shina