Storm FM

GGM Kili Challenge 2025 yazinduliwa

18 July 2025, 5:06 pm

Viongozi mbalimbali wa serikali na mgodi wa GGML wakiwa kwenye picha ya pamoja ya uzinduzi.Picha na Mwandishi wetu

Tangu kuanzishwa kwa Kili Challenge mwaka 2002 imelenga kukusanya Dola za Kimarekani Milioni Moja kila mwaka.

Na Mwandishi Wetu:

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu Mhandisi Jackson Masaka leo Julai 18,2025 ameongoza zoezi la uzinduzi wa GGM Kili Challenge 2025 katika Lango la Machame wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro.

Akizungumza katika hafla hiyo mhandisi Jackson amesema amewapongeza Jumla ya washiriki 67 walioshiriki kwa mwaka huu ikijumuisha Wapanda mlima 47  na waendesha baiskeli 17 kwa ushiriki wao kwa mwaka huu ambapo  wamekabidhiwa  bendera kwa ajili ya kuanza shughuli ya kupanda mlima safari  inayoashiria  kuanza kwa safari  ya kishujaa  “Paa la Afrika” kwa ajili ya kuunga mkono mapambano ya kitaifa dhidi ya VVU na UKIMWI

Viongozi mbalimbali wa serikali na mgodi wa GGML wakiwa kwenye picha ya pamoja ya uzinduzi.Picha na Mwandishi wetu

Akiwa katika hafla hiyo Makamu wa Rais wa AngloGold Ashanti wa Masuala ya Uendelevu na Mambo ya Ubia (Afrika), Simon Shayo, amesema GGM Kili Challenge ni harakati inayoonyesha nguvu ya umoja na dhamira ya kumaliza VVU/UKIMWI katika jamii nakueleza baadhi ya miradi wanayoitekeleza hasa katika mkoa wa Geita. 

Amesema kuwa Fedha zitakazochangwa kupitia tukio hili zitaelekezwa moja kwa moja katika shughuli za kuzuia, kupima, kutibu, kuhudumia na kuelimisha kuhusu VVU/UKIMWI kupitia Kili Challenge Trust Fund, ikinufaisha maelfu ya Watanzania kote nchini

Wananchi na washiriki mbalimbali wa GGM Kili Challenge wakiwa kwenye uzinduzi. Picha na mwandishi wetu

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TACAIDS, Yasin Absa, amepongeza ushirikiano wa muda mrefu na GGML, na kueleza takwimu za maambukizi ya virusi vya ukimwi nchini na njia amabazo zinaendelea kutumika kutokomeza virusi vya ukimwi

Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2002, Kili Challenge imelenga kukusanya Dola za Kimarekani Milioni Moja kila mwaka, na imechangia kwa kiasi kikubwa katika programu za UKIMWI zinazotegemea jamii, hasa katika maeneo ambayo ni vigumu kufikika.

Sauti ya mwandishi wetu Ashura Ramadhani akifafanua zaidi