Storm FM

NMB yawa mkombozi kwa walimu Geita

14 July 2025, 7:35 pm

Walimu kutoka wilayani Geita wakiwa kwenye uzinduzi wa Program ya mwalimu Special mjini Geita.Picha na Mrisho Sadick

Benki ya NMB imeendelea kuwa karibu na walimu ili kuwapunguzia baadhi ya changamoto ambazo ziko ndani ya uwezo wa benki hiyo kama mikopo yenye mashariti nafuu.

Na Mrisho Sadick:

Serikali imeahidi kuendeleza ushirikiano na Benki ya NMB kutokana na mchango wake mkubwa katika kuwathamini na kuwaheshimu walimu kwa kutambua nafasi yao muhimu katika jamii.

Ahadi hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe Martine Shigela wakati wa ufunguzi wa Programu ya Mwalimu Special uliofanyika Julai 14, 2025, mjini Geita Programu ambayo inaratibiwa na Benki ya NMB.

Sauti ya Mkuu wa mkoa wa Geita
Mkuu wa Mkoa wa Geita Martine Shigela akiwa katika uzinduzi wa programu ya Mwalimu Special. Picha na Mrisho Sadick

Walimu zaidi ya 300 kutoka wilayani  Geita wameungana kushiriki programu hiyo inayolenga kuwajengea uwezo, kuboresha afya, kuwawezesha kiuchumi na kuwaandaa kwa maisha bora kazini na baada ya kustaafu.

Meneja wa NMB Kanda ya Ziwa, Faraja Mg’ingo, amesema lengo kuu ni kuwatambua walimu kama nguzo ya maendeleo ya taifa kwa kuwapa elimu ya kifedha, mikopo nafuu ya makazi na kuwahamasisha kutumia fursa mbalimbali za benki hiyo.

Sauti ya meneja wa kanda NMB
Meneja wa Benki ya NMB kanda ya ziwa akizungumza katika uzinduzi wa programu ya Mwalimu Special. Picha na Mrisho Sadick

Walimu waliopata fursa hiyo wamesema elimu waliyoipata itawasaidia kupanga maisha yao kwa ufanisi zaidi, huku wakifurahishwa na namna ambavyo NMB inawaunga mkono kwa vitendo nakwamba kaulimbiu ya “Umetufunza, tunakutunza”, imeibuka kuwa kielelezo cha namna taasisi binafsi zinavyoweza kushiriki katika maendeleo ya sekta ya elimu kwa kuwajali wale wanaoijenga.

Sauti za walimu