Storm FM

Madereva Shilabela wapinga kuondolewa eneo la kupaki

12 July 2025, 5:01 pm

Madereva wa magari ya mizigo wakiwa katika eneo ambalo wanatakiwa kuondoka. Picha na Kale Chongela

Kutimuliwa kwa madereva wa mizigo eneo lao la kupaki Shilabela Manispaa ya Geita lachukua sura mpya

Na Kale Chongela:

Madereva wa magari ya mzigo yanayopaki pembezoni mwa barabara katika Mtaa wa Shilabela Kata ya Buhalahala  Manispaa ya Geita Mkoani Geita wamepinga kauli ya mwenyekiti wa serikali ya mtaa huo ya kuwataka kuondoka katika eneo hilo bila sababu za msingi.

Wakizungumza  na Storm FM baadhi ya madereva hao wamebainisha kuwa wamekuta kuna bango linalodaiwa kuwekwa na mwenyekiti wa serikali ya mtaa huo lakuwataka kuondoka katika eneo hilo huku wakisema hawawezi kuondoka hadi pale serikali itakapo watafutia eneo lingine kwa ajili ya kupaki magari yao.

Sauti ya madereva wa magari ya mizigo
Madereva wa magari ya mizigo wakiwa katika eneo ambalo wanatakiwa kuondoka. Picha na Kale Chongela

Mlinzi wa magari hayo Bw RobartWest  amesema  baada ya kufika katika eneo hilo alikuta bango  lenye maandishi  yanayosomeka ni maarufuku kupaki magari eneo hili jambao ambalo yeye binafsi limempa wakati mgumu 

Sauti ya mlinzi wa magari ya mizigo

Mwenyekiti  wa Serikali ya Mtaa huo Bw Fredrick Masalu  amekiri kuweka bango hilo na kwamba ni kutokana na magari yanayopaki eneo hilo kuwa chanzo cha uchafuzi wa mazingira  sambamba na uwepo wa madalali wanaoingiza kipato kupitia magari hayo kwa maslahi yao binafsi.