Storm FM

Wananchi waanzisha ujenzi wa soko Mbogwe

12 July 2025, 4:43 pm

Baadhi ya wanawake wa Mji Mwema wakiwa katika zoezi la kusafisha eneo la ujenzi wa soko. Picha na Edga Rwenduru

kutembea umbali mrefu , ajali za barabarani zimewasukuma wakazi wa Mji Mwema kuanzisha ujenzi wa soko la mtaa

Na Edga Rwenduru:

Wakazi wa Kitongoji cha Mji Mwema Kata ya Lulembela wilayani Mbogwe Mkoani Geita wameamua kuanzisha Ujenzi wa soko la Kitongoji hicho ili kuepukana na Changamoto ya kutembea umbali mrefu pamoja na ajali wakati wa kuvuka Barabara kuelekea soko la Lulembela kufuata huduma.

Ujenzi wa soko hilo umepitishwa kupitia mikutano halali ya Kitongoji hicho huku Wananchi wakielezea furaha hayo pindi soko hilo litakapo kamilika nakuanza kutoa huduma huku wakiiomba serikali na wadau wa maendeleo kuwashika mkono ili kukamilisha kazi hiyo kwa wkati.

Muonekano wa baadhi ya miundombinu ya soko la mtaa wa Mji Mwema. Picha na Edga Rwenduru
Sauti Wananchi

Katibu wa Kamati ya Maendeleo ya Kitongoji hicho amesema walikubaliana kila kaya kuchangia shilingi Elfu 10,500 kwa ajili ya ujenzi wa soko hilo nakwamba wamenunua Ardhi yenye ukubwa wa ekari mbili kwa ajili ya soko hilo.

Sauti ya katibu wa maendeleo ya mtaa

Mwenyekiti wa kitongoji cha Mji Mwema Mashaka Mawengaya amesema Mapato yote yatakayopatikana katika soko hilo yatasaidia ununuzi wa chakula katika shule ya msingi Magufuli.

Sauti ya mwenyekiti wa mtaa