Storm FM

Upandishaji nauli holela bado changamoto Geita

21 June 2025, 2:24 pm

Baadhi ya magari ya abiria yakiwa kwenye kituo kikuu cha mabasi ya abiria Mkoani Geita. Picha na Edga Rwenduru

Suala la upandishaji nauli holela bado ni kizungumkuti katika kituo kikuu cha mabasi ya abiria mjini Geita

Na Edga Rwenduru:

Jeshi la Polisi kikosi cha usalama barabarani wilaya ya Geita kwa kushirikiana na mabalozi wa usalama barabarani mkoa wa Geita wamebaini idadi kubwa ya mabasi ya abiria yanayofanya safari za Geita -Kagera kuwazidishia nauli abiria na baadhi ya mabasi kushindwa kutoa tiketi mtandao kwa abairia.

Akizungumza wakati wa Oparesheni iliyofanywa na Mabalozi wa usalama barabarani mkoa wa Geita kwa kushirikiana na polisi kitengo cha usalama barabarani katika stendi kuu ya Mabasi ya Abiria  Kaimu Afisa mfawidhi RATRA Mkoa wa Geita Mukiya Juma Manyanga amesema waliokutwa na makosa hayo wamepigwa faini ya laki mbili na nusu.

Sauti ya kaimu mfawidhi wa LATRA
Mabalozi wa usalama barabarani wakiwa na jeshi la polisi katika ukaguzi wa magari ya abiria. Picha na Edga Rwenduru

Kwa upande wake kaimu mkuu wa kikosi cha usalama barabarani wilaya ya Geita Phabiano Daniel amesema madereva wote wanaoendesha kwa mwendo kasi zaidi ya 99 wanafungiwa leseni kwa miezi mitatu.

Sauti ya kaimu RTO Geita
Kaimu mkuu wa kikosi cha usalama barabarani wilaya ya Geita Phabiano Daniel akizungumza na Storm FM. Picha na Edga Rwenduru

Odasi Ngoma na Joseph Mugire ni viongozi wa Mabalozi wa usalama barabarani wamesema changamoto kubwa ambayo ipo magari mengi hayana mikanda na wahudumu wa magari hayo hawatoi tiketi mtandao kwa abiria

Sauti ya viongozi wa mabalozi wa usalama barabarani