Storm FM

Nyang’hwale yapata hati safi miaka 5 mfululizo

12 June 2025, 3:56 pm

Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye kikao cha baraza maalumu la madiwani la Halmashauri ya Nyangla kujadili hoja za CAG. Picha na Mrisho Sadick

Halmashauri ya wilaya ya Nyang’hwale imeendelea kupata hati safi kutoka kwa mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG

Na Mrisho Sadick:

Kaimu mkuu wa mkoa wa Geita ambae ni mkuu wa mkoa wa Kagera Hajat Fatma Mwasa amewataka watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Nyang’hwale Mkoani Geita kuongeza ufanisi katika usimamizi , ufuatiliaji na uwajibikaji wa shughuli mbalimbali za serikali Ili kupunguza au kumaliza kabisa hoja za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG).

Hajat Fatma Mwasa ametoa kauli hiyo kwenye mkutano maalumu wa baraza la madiwani wa Halmashauri ya wilaya hiyo la kujadili majibu ya hoja na mpango kazi wa utekelezaji wa mapendekezo ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG kwa  mwaka wa fedha 2023/2024 huku mkuu wa wilaya hiyo Grace Kingalame akimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha nyingi kwa ajili ya miradi ya maendeleo katika wilaya hiyo.

Sauti ya kaimu mkuu wa mkoa Geita na Mkuu wa wilaya ya Nyang’hwale

Akiwa kwenye baraza hilo Mkaguzi mkuu wa nje wa hesabu za serikali Mkoa wa Geita Waziri Shaban amesema  halmashauri hiyo imeendelea kuweka rekodi ya kupata hati safi kwa miaka mitano mfululizo kuanzia mwaka fedha 2019/2020 hadi 2023/2024 huku akiwataka madiwani kuongeza msukumo kwa baadhi ya mambo ambayo wanaona hayaendi sawa sawa.

Kaimu mkuu wa mkoa wa Geita akihutubia baraza la madiwani Nyang’hwale. Picha na Mrisho Sadick
Sauti ya Mkaguzi wa nje Geita
Viongozi wakiwa kwenye kikao cha baraza maalumu la madiwani la Halmashauri ya Nyangla kujadili hoja za CAG. Picha na Mrisho Sadick

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Husna Toni ameahidi kufanyia kazi maagizo na mapendekezo yote yaliyotolewa kwenye baraza hilo huku mwenyekiti wa Halmashauri hiyo John Isack akisisitiza kila mtumishi kuendelea kuwajibika kwa nafasi yake ili kumaliza hoja hizo.

Sauti ya Mkurugenzi na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Nyan’gwale