Storm FM

Maduka manne yavunjwa, mali zaibiwa mtaa wa Mbugani

15 May 2025, 5:22 pm

Sehemu ya eneo la mtaa wa Mbugani ambapo wizi umefanyika. Picha na Kale Chongela

‘Tunaendelea kumshikilia meneja wa kampuni inayolinda hapa ili aweze kutoa ushirikiano wa kubaini waliokuwa zamu ya usiku’ – Mwenyekiti wa mtaa

Na: Kale Chongela:

Maduka manne ya wafanyabiashara katika mtaa wa Mbugani kata ya Kalangalala, halmashauri ya manispaa ya Geita yamevunjwa na bidhaa zilizokuwemo ndani kuibiwa.

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia Mei 14, 2025 akizungumza Mwenyekiti wa wafanyabiashara katika eneo hilo Bw. Rwegasila Philibert amesemamajira ya saa kumi usiku ndipo alipata taarifa juu ya wizi huo ambapo alianza jitihada za kumtafuta meneja wa kampuni  ambayo ilikuwa ikilinda eneo hilo.

Sauti ya mwenyekiti wa wafanyabiashara Mbugani

Msimamizi wa kampuni ya Binson inayohusika na ulinzi eneo lililovunjwa  James Kitulo amekiri wizi kufanyika ambapo amesema  jitihada zinaendelea za kuwatafuta walinzi ambao walikuwa zamu huku akiahindi kulipa gharama zote zilizotokana na wizi huo.

Sauti ya msimamizi wa kampuni ya ulinzi
Baadhi ya wananchi wakazi wa mtaa wa Mbugani waliojitokeza kushuhudia. Picha na Kale Chongela

Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Mbugani Jumanne Bayasabe amemshikilia msimamizi huyo ili aweze kutoa ushirikianao ikiwemo kufahamu waliokuwa wanalinda eneo hilo.

Sauti ya mwenyekiti wa serikali ya mtaa Jumanne Bayasabe

Afisa Mtendaji wa kata ya Kalangalala Bw. Hamad Hussein amethibitisha kutokea kwa tukio na kuitaka kampuni hiyo kutenda haki ikiwemo wafanyabiashara kulipwa fidia zao.

Sauti ya afisa mtendaji kata ya Kalangalala Hamad Hussein