Storm FM

Ubovu wa barabara hospitali Katoro

13 April 2025, 1:56 pm

Muonekano wa ubovu wa barabara ya Hospitali ya Katoro. Picha na Mrisho Sadick

Ubovu wa barabara ya kwenda katika hospitali ya Katoro wawaibua wananchi wa kata za Katoro na Ludete wawaibua wananchi

Na Mrisho Sadick:

Wakazi wa Kata ya Ludete mamlaka ya mji mdogo wa Katoro wilayani Geita wameiomba serikali kuchukua hatua za haraka kutengeneza barabara inayoelekea kwenye Hospitali ya Katoro kutokana na barabara hiyo kuharibika vibaya.

Muonekano wa baadhi ya majengo ya Hospitali ya Katoro. Picha na Mrisho Sadick

Wananchi hao wametoa kilio hicho wakati wakizungumza na Channel Ten ambapo wamesema  wanapata changamoto kuwafikisha wagonjwa kwenye  hospitali hiyo  kutokana na barabara zote zinazoingia eneo hilo kuharibiwa vibaya na mvua zinazoendelea kunyesha. 

Sauti ya wananchi
Mwenyekiti wa CCM akizungumza na meneja TARURA kwa njia ya simu. Picha na Mrisho Sadick

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita Nicholous Kasendamila amefika katika Hospitali hiyo kuangazia changamoto hiyo nakumuagiza  Meneja wa TARURA wilaya ya Geita Mhandisi Bahati Subeya  kwa njia ya simu kuhakikisha anatatua changamoto hiyo haraka.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita