Storm FM

Mzee alalamika kunyimwa huduma za afya Kasota

4 April 2025, 2:39 pm

Mzee Ernest Gabriel katika tabasamu baada ya kupewa barua ya matibabu bila malipo. Picha na Mrisho Sadick

Serikali inatakiwa kuweka mkazo kwenye utatuzi wa changamoto ya matibabu bila malipo kwa wazee kwani wengi wao wamekuwa wakikosa fursa hiyo.

Na Mrisho Sadick:

Mzee Ernest Gabriel Mkazi wa Kijiji cha Kasota Kata ya Bugulula wilayani Geita  anaesumbuliwa na maradhi kwa muda mrefu amedai kufukuzwa nakunyimwa huduma kwenye Kituo cha Afya Kasota kwa madai kuwa hana barua Kutoka Ofisi ya Mtendaji wa Kijiji hicho.

Mzee Gabriel anaeishi katika mazingira magumu ametoa malalamiko hayo April 04,2025 kwenye Mkutano wa hadhara wa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita aliyefika kwenye Kijiji hicho kusikiliza nakutatua kero za wananchi huku akihoji Kwanini hapewi huduma bure licha ya serikali kusisitiza wazee kutibiwa bila malipo.

Sauti ya Mzee Gabriel
Wakazi wa Kasota wakiwa kwenye mkutano wa mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita. Picha na Mrisho Sadick

Mganga mfawidhi wa Kituo Cha Afya Kasota Dkt Enos Jumanne amekiri kumtambua Mzee huyo nakwamba hakuwapatiwa huduma kwenye Kituo hicho kwakuwa hana barua Kutoka Ofisi ya Mtendaji wa Kijiji.

Sauti ya Mganga mfawidhi
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita akizungumza na wakazi wa kijiji cha Kasota Kata ya Bugulula. Picha na Mrisho Sadick

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita Nicholaus Kasendamila akamtaka Mtendaji wa Kijiji hicho kumpatia barua Mzee huyo kwenye Mkutano huo Ili awe kwenye Mpango wa wazee wanaopatiwa huduma bila malipo huku akimuagiza Mkuu wa wilaya ya Geita kusimamia suala hilo.

Sauti ya mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita