Storm FM

Adaiwa kunywa sumu baada ya mke kuondoka na Tsh. laki 2

21 March 2025, 10:45 am

Gerevas Deus akihojiwa katika ofisi ya serikali ya mtaa wa Mpomvu.

Mwanaume mmoja mkazi wa kata ya Kasamwa katika halmashauri ya manispaa ya Geita amenusurika kifo baada ya kufanya jaribio la kujiua kwa kunywa sumu.

Na: Kale Chongela – Geita

Gerevas Deus anakadiriwa kuwa na umri wa miaka 28 mkazi wa kijiji cha  Mbugani  kata ya Kasamwa, halmashauri ya manispaa ya Geita amenusurika kifo baada ya kufanya jaribio la kunywa sumu baada ya mke wake kutoweka nyumbani waliopokuwa wanaishi.

Baadhi ya ndugu wa mke wake wakiwa katika ofisi ya serikali ya mtaa wamesema kijana huyo alikwenda nyumbani kwao na mke wake waishio mtaa wa Mpomvu ili kuulizia kama amekwenda huko.

Mtuhumiwa na wanafamilia ya mke wa mtuhumiwa wakiwa ofisi ya serikali ya mtaa.

Baada ya kugundua kuwa mkewe hajafika nyumbani kwao ndipo akaamua kuchukua uamuzi wa kunywa sumu akiwa katika mtaa huo kama anavyoeleza mama mzazi wa mke wake.

Sauti ya mama mzazi wa mke B. Roza Msija

Balozi wa shina 3 katika mtaa wa Mpomvu Bw. Andrea Machibula ameeleza namna alivyopata taarifa juu ya tukio hilo.

Sauti ya Balozi Bw. Andrea Machibula

Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Mpomvu Bw. Charles Manyanga amethibitidha kutokea  tukio hilo na kwamba baada ya kijana huyo kuhojiwa amekiri kuwa alikunywa sumu mara baada ya kugundua kuwa mke wake wakati anaondoka alichukua kiasi cha fedha za kitanzania shilingi Laki mbili jambo ambalo kwake lilimpa wakati mgumu.

Sauti ya mwenyekiti wa mtaa Bw. Charles Manyanga