Storm FM

COPRA yakabidhi zaidi ya tani 50 za mbegu za alizeti Geita

5 March 2025, 12:27 pm

Mkuu wa mkoa wa Geita Martine Shigela akizungumza na wana habari. Picha na Daniel Magwina

Hadi kufikia Desemba 2022 jumla ya wakulima 6,323 na eneo la ekari 11,896 lilikuwa limetengwa kwa ajili ya kilimo cha alizeti Geita, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuongeza uzalishaji na kujitosheleza kwa mafuta ya kula nchini.

Na: Daniel Magwina – Geita

Mamlaka ya Nafaka na Mazao mchanganyiko nchini (COPRA) imekabidhi zaidi ya tani hamsini za mbegu za alizeti mkoani Geita kwa ajili ya kugawiwa kwa wakulima mkoani Geita bure.

Ugawaji huo umefanyika Machi 04, 2025. Akizungumza mwakilishi wa Mkurugenzi wa mamlaka hiyo Bi. Sezaria Makota wakati akikabidhi mbegu hizo kwa mkuu wa mkoa wa Geita amesema:

Sauti ya mwakilishi kutoka COPRA Bi. Sezaria Makota
Mwakilishi kutoka COPRA Bi. Sezaria Makota akizungumza na wana habari. Picha na Daniel Magwina

Akizungumza baada ya kupokea mbegu hizo Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martin Reuben Shigela amewapongeza COPRA kwa kuleta mbegu bora kwa wakulima kwa ajili ya zao la alizeti

Sauti ya Mkuu wa Mkoa wa Geita Martine Shigela

Akizungumza kwa niaba ya wakuu wa wilaya wa mkoa wa Geita, Mkuu wa Wilaya ya Geita Hashim Komba amesema watahakikisha wakulima wanapata mbegu hizo ili ziweze kuleta tija iliyo kusudiwa.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Geita Hashim Komba

Nao baadhi ya wakulima lutokea wilaya mbalimbali mkoani hapa wameelezea jinsi watakavo simamia mbegu hizo.

Sauti ya wakulima
Mifuko yenye mbegu za Alizeti ambazo zimetolewa kwa wakulima wa Geita. Picha na Daniel Magwina