Storm FM

Auawa kwa madai ya wizi wa ng’ombe Geita

10 February 2025, 11:53 am

Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Iponyamakalai eneo ambalo mtuhumiwa ameuawa. Picha na mwandishi wetu

Vitendo vya wizi wa mifugo aina ya ng’ombe vinaendelea kuchukua sura mpya mkoani Geita ambapo matukio hayo yameendelea kujitokeza hali inayochochea hasira za wananchi.

Na: Amon Mwakalobo – Geita

Mwanaume mmoja anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 45 ameuawa na wananchi wenye hasira kali katika kitongoji cha Kasenyi, kata ya Nyakamwaga,  kijiji cha Iponyamakalai wilayani na mkoani Geita baada ya kukutwa akiwa na nyama ndani ya mifuko  akisadikiwa kushirikiana na baadhi ya watu kuchinja ng’ombe wanaodaiwa kuibwa kutoka kwenye kaya ya mmoja wa wananchi katika kijiji hicho.

Tukio hilo limetokea alfajiri ya kuamkia februari  08, 2025 ambapo kwa mujibu wa Mwenyekiti wa kitongoji hicho amesema alipigiwa simu na wananchi kumueleza juu ya tukio hilo, huku akitupa lawama kwa watu wanaofanya vitendo vya wizi.

Sauti ya mwenyekiti wa kitongoji
Mifuko iliyohifadhi nyama ambayo ilikuwa imepatikana baada ya kuchinja. Picha na mwandishi wetu

Sikudhani Shija ni mke katika familia iliyoibiwa mifugo yao ambapo anaeleza namna alivyofahamu juu ya tukio hilo.

Sauti ya mmiliki wa ng’ombe Bi. Sikudhani Shija

Jirani wa familia iliyoibiwa Mariam Bugalama ameeleza namna alivyosikitishwa na tukio hilo akieleza kuwa matukio hayo yamekuwa ya kujirudia kila siku katika eneo hilo.

Sauti ya Jirani Bi. Mariam Bugalama

Mmoja wa shuhuda wa tukio hilo Banza Luchapa ameeleza namna alivyoshuhudia juu ya tukio hilo ambapo anaeleza ilikuwa majira ya saa tisa usiku.

Sauti ya shuhuda Bw. Banza Luchapa

Storm FM tunaendelea na jitihada za kumtafuta kamanda wa polisi mkoa wa Geita kufahamu mikakati ya Jeshi la polisi katika kukabiliana na vitendo vya wizi mkoani Geita.