Storm FM

Migogoro ya ndoa ni kikwazo kwa wakazi wa Kaseme

4 February 2025, 12:32 pm

Wananchi wa kata ya Kaseme wakipewa elimu ya sheria juu ya ndoa. Picha na Kale Chongela

Februari 03, 2025 imehitimishwa wiki ya sheria nchini ambapo sambamba na hilo pia msaada wa kisheria wa Mama Samia Legal Aid umekamilika katika mkoa wa Geita.

Na: Kale Chongela – Geita

Migogoro  ya ndoa katika kijiji cha kaseme, halmashauri ya wilaya ya Nyang’hwale, mkoani Geita imetajwa kuwa chanzo cha kudidimiza uchumi wa familia pindi inapojitokeza.

Hayo yamebainishwa na baadhi ya wanawake wa kijiji  hicho katika mkuatano wa hadhara katika hitimisho la kampeni ya msaada wa kisheria wa mama samia ambapo wameeleza chanzo kikubwa ni wanaume kuzaa nje ya ndoa hali ambayo inaondoa maelewano katika familia

Sauti ya wanawake

Baadhi ya wanaume wameeleza kuwa migogoro ya familia inachochewa na vitu vingi ikiwemo mfumo dume pamoja na vikundi mbalimbali ambavyo hurubuni baadhi ya wanawake na kupelekea mabadiliko yao kitabia.

Sauti ya wanaume

Mwenyekiti  wa serikali ya kijiji cha Kaseme Bw. Michael Kashindye amekiri uwepo kwa migogoro  ya kifamilia  katika kijiji chake akieleza kuwa elimu iliyotolewa uitasaidia kuweza kuepusha migogoro hiyo.

Sauti ya mwenyekiti kijiji cha Kaseme Michael Kashindye

Kwa upande wake wakili msomi kutoka timu ya wataalamu wa kampeni ya msaada wa kisheria  ya Mama Samia Bw Yessey Lubunda  amesema matatizo mengi katika Jamii huanzia katika ngazi ya familia na hivyo kupitia kampeni hiyo itakuwa chachu ya kleta mabadiliko

Sauti ya wakili msomi Yessey Lubunda