Storm FM

TEHAMA yaongeza kasi uendeshaji shughuli za Mahakama Geita

3 February 2025, 5:12 pm

Jaji mfawidhi wa mahakama kuu kanda ya Geita Kelvin Mhina katika maadhimisho ya siku ya sheria. Picha na Ester Mabula

Kilele cha wiki ya sheria nchini hufanyika kwa kujumuisha shughuli mbalimbali zinazohusiana na masuala ya sheria ili kuelimisha wananchi na kuhamasisha matumizi bora ya sheria katika jamii.

Na: Ester Mabula – Geita

Jaji mfawidhi wa mahakama kuu kanda ya Geita Kelvin Mhina amesema mashauri zaidi ya elfu nane sawa na asimilia 94.2 yamesikilizwa na kukamilishwa kwa mwaka 2024 ikiwa ni miongoni mwa malengo waliyojiwekea ya kumaliza kesi zote kwa wakati na kwa viwango vya juu zaidi.

Jaji Mhina ameyasema hayo leo februari 03, 2025 katika kilele cha maadhimisho ya siku ya sheria nchini yaliyofanyika katika viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan zamani EPZA mkoani Geita ambapo amesema matumizi ya TEHAMA katika shughuli za mahakama yamesaidia kwa kiasi kikubwa mafanikio hayo kwani ndio ukuaji wa teknlojia.

Sauti ya Jaji mfawidhi mahakama kuu kanda ya Geita

Mkuu wa mkoa wa Geita Martine Shigela amesema serikali itaendelea kuboresha mifumo zaidi ili kurahisisha shughuli za kimahakama sambamba na kuweza kuwasaidia watanzania juu ya masuala mbalimbali kuhusu haki.

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Geita Martine Shigela
Mkuu wa mkoa wa Geita Martine Shigela katika maadhimisho siku ya sheria. Picha na Ester Mabula

Katika hatua nyingine RC Shigela amewataka waandishi wa habari kuandika habari za kesi za madai kwa uwazi bila kuogopa usalama wao kwani atahakikisha analinda usalama wao

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Geita Martine Shigela
Watumishi wa sekta mbalimbali ikiwemo mahakama katika maadhimisho ya siku ya sheria. Picha na Ester Mabula

Kauli mbiu mbiu katika maadhimisho ya kilele cha siku ya sheria nchini ni TANZANIA YA 2050: NAFASI YA TAASISI ZINAZOSIMAMIA HAKI MADAI KATIKA KUFIKIA MALENGO MAKUU YA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO

Watumishi wa sekta mbalimbali ikiwemo mahakama katika maadhimisho ya siku ya sheria. Picha na Ester Mabula