Storm FM

Rais Samia atoa milioni 50 kwa wanawake Geita

22 October 2024, 9:59 pm

Mkuu wa mkoa wa Geita akimkabidhi mwenyekiti wa taasisi ya wanawake na Samia risiti ya fedha zilizotolewa na Rais Dkt Samia. Picha na Mrisho Sadick

Serikali imeendelea kuweka nguvu kwa wanawake wanaofanya shughuli katika migodi ya uchimbaji wa madini ya dhahabu ili kuwainua kiuchumi.

Na Mrisho Sadick:

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassani ametoa kiasi cha shilingi milioni 50 kwa taasisi ya Wanawake na Samia mkoa wa Geita kwa lengo la kuwaongezea mtaji wa kuendeleza biashara yao ya kupika chakula kwa wafanyakazi wa Shirika la Madini la Taifa STAMICO katika mgodi wa GGML.

Akikabidhi risiti za kiasi cha fedha kilichowekwa katika akaunti ya taasisi hiyo na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Samia Sukuhu Hassan Oktoba 21,2024 Mkuu wa mkoa wa Geita Martine Shigela amewataka kutumia fedha hizo kwa malengo yaliyokusudiwa ili kukuza mtaji na kupanua wigo wa kutoa huduma ya chakula kwa makampuni mengine.

Sauti ya Mkuu wa mkoa wa Geita

Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Adelina Kabakama amesema wanatoa huduma ya chakula kwa watumishi zaidi ya 100 wa shirika la madini la taifa STAMICO ambapo wamemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwasaidia kutatua changamoto ya mtaji.

Sauti ya Viongozi wa taasisi ya wanawake na samia
Viongozi wa taasisi ya wanawake na samia mmoa wa Geita wakiwa katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Geita. Picha na Mrisho Sadick

Hivi karibuni akiwa mkoani Geita kwenye hafla ya kufunga maonesho ya saba ya teknolojia na uwekezaji katika sekta ya madini Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan aliahidi kuendelea kuwashika mkono wanawake wanaofanya kazi migodini.

Sauti ya Rais Dkt Samia akiwa Mkoani Geita