Storm FM

Wakazi Buhalahala wapongeza uwekwaji taa za barabarani

28 September 2024, 10:27 am

Moja ya taa za barabarani ambazo zimewekwa katika kata ya Buhalahala. Picha na Kale Chongela

Mkoa wa Geita umeendelea kukua na kuimarika kupitia nyanja mbalimbali, hivyo uboreshaji wa miundombinu ni muhimu katika ukuaji wa uchumi.

Na: Kale Chongela – Geita

Wakazi wa kata ya Buhalahala halmashuri ya mji wa Geita  wameipongeza serikali kwa kuendelea kuboresha miundombinu kwa kuweka taa pembezoni mwa barabara kuu.

Shughuli mbalimbali za barabarani zikiendelea halmashauri ya mji wa Geita. Picha na Kale Chongela

Wakizungumza Septemba 27, 2024 baadhi ya wakazi wa mtaa wa Mwatulole uliopo katika kata hiyo wamesema kuwepo kwa taa hizo zitawasaidia wananchi wa eneo hilo hasa watembea kwa miguu.

Sauti ya wananchi

Aidha wananchi wameendelea kueleza kuwa taa hizo ni chachu kubwa katika hatua ya ukuaji wa kiuchumi kwa mkoa na taifa  kwa ujumla.

Sauti ya mwananchi

Akizungumza kwa njia ya simu mtaalumu kutoka wakala wa Barabara mkoani  Geita (TANROADS) Mhandisi Fedrick Mande amesema ili taa hizo ziweze kudumu kwa muda ipo haja kwa kila mwananchi kutoa ushirikiano katika kulinda miundombinu ya barabara ili kuepukana na hasara zisizokuwa za lazima.

Sauti ya mhandisi