Storm FM

TAMISEMI yatoa maagizo kwa mkandarasi Geita

1 September 2024, 9:11 pm

Moja kati ya mitambo ya mkandarasi anayefanya ujenzi wa barabara ya miradi ya TACTIC Geita mjini. Picha na Evance Mlyakado

Kusuasua kwa mkandarasi anaetekeleza ujenzi wa mradi wa TACTIC wa barabara zenye urefu wa kilometa 17 TAMISEMI yatoa tamko.

Na Evance Mlyakado – Geita.

Licha ya serikali kutenga bajeti ya zaidi ya bilioni 22 kwaajili ya ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilometa 17 kwa kiwango cha lami katika kata nne zilizopo mjini Geita bado ujenzi wa mradi huo unasuasua kutokana na mkandarasi anayetekeleza mradi huo kushindwa kuendana na kasi inayotakiwa kwa mujibu wa mkataba.

Mradi huo unaotekelezwa kupitia ufadhili wa benki ya dunia unapaswa kukamilika ndani ya miaezi 15 ambapo mpaka sasa miezi tisa imepita lakini bado mradi huo umetekelezwa kwa asilimia 34 jambo ambalo limepelekea naibu katibu mkuu wa ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia miundombinu Mhandisi Rogatus Mativila kufika katika mradi huo na kumuagiza mkandarasi kukamilisha mradi huo kabla ya mwezi februari 2025.

Sauti ya naibu katibu mkuu TAMISEMI Mhandisi Rogatus Mativila

Daraja lililopo mtaa wa uwanja eneo la kivukoni likiendelea kujengwa ni miongoni mwa barabara iliyopo katika mradi wa TACTIC. Picha na Evance Mlyakado.

Kwa upande wake Mkurugenzi anayesimamia mradi huo katika mji wa Geita Mhandisi Lukasi Nyake  amesema mkandarasi huyo ameshapatiwa ushauri wa kitaalamu zaidi ya mara 45 lakini bado hali ya mwenendo wa mradi huo inaendelea kuwa mbaya.

Sauti ya mkurugenzi anayesimamia mradi Mhandisi Lukas Nyake

Moja ya barabara zilizopo kwenye mradi wa TACTIC Geita mjini. Picha Evance Mlyakado

Nao wananchi wamebainisha changamoto wanazozipata kutokana na mradi huo kutokamilika  kwa wakati.

Sauti za wananchi