Storm FM

Wakazi Nyarugusu walalamika ujenzi wa barabara kusimama

1 August 2024, 2:17 am

Muonekano wa barabara ambayo imesimama ujenzi wake eneo la Nyarugusu. Picha na Kale Chongela

Wakazi wa kata ya Nyarugusu Wilaya ya Geita wamelalamikia hali ya kusimama kwa ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilomita moja.

Na: Kale Chongela – Geita

Malalamiko ya wanachi hao yamekuja kufuatia usumbufu ambao wananchi hao wanaeleza kuupata hususani watumiaji wa vyombo vya moto.

Wameeleza hayo Julai 30, 2024 wakati wakizungumza na Storm Fm ambapo wameeleza kuwa ni zaidi ya siku 60 ujenzi huo umesimama jambo ambalo linawapa wakati mgumu.

Baadhi ya madereva wa boda boda katika eneo hilo wanaeleza kuwa baada ya ujenzi huo kusimama barabara imefugwa huku akiiomba serikali kufungua barabara hiyo ili iweze kuwarahisishia kazi yao.

Sauti ya madereva

Oscar Fredrico ni katibu wa egesho la bodaboda la Nyarugusu anaiomba serikali kuweza kufungua barabara hio ili kuwasaidia watumiaji kuondokana na changamoto ya sasa.

Sauti ya katibu

Kutoka wakala wa barabara TANROADS  mkoa wa Geita mhandisi  Fredrick Mande akizungumza kwa njia ya simu amesema barabara hiyo ina urefu wa kilomota 1 na miongoni mwa sababu zilizopelekea kusimama kwa ujenzi huo ni fedha kuchelewa hali iliyopelekea mkandarasi kusimama kwa muda hadi fedha itakapopatikana ndipo ujenzi utaendelea.

Sauti ya mhandisi