Storm FM

Kata ya Ihanamilo yakabiliwa na uhaba wa maji

13 July 2024, 12:38 pm

Afisa elimu kata ya Ihanamilo akitoa ufafanuzi kwa mbunge wa Geita mjini Constantine Kanyasu baada ya kufanya ziara eneo hilo. Picha na Edga Rwenduru

Licha ya serikali kufanya jitihada za ujenzi wa matundu ya vyoo katika shule zilizopo kata ya Ihanamilo, eneo hilo linakabiliwa na changamoto ya uhaba wa maji.

Na: Edga Rwenduru – Geita

Changamoto ya uhaba wa maji katika kata ya Ihanamilo halmashauri ya mji wa Geita inapelekea wanafunzi kushindwa kufanya usafi wa vyoo vya shule kwa wakati na kuwaweka hatarini kupata magojwa ya mlipuko.

Hayo yamebainishwa na afisa elimu kata ya Ihanamilo Simon Shija na diwani wa kata hiyo Joseph Rugahila Julai 11, 2024 wakati wa ziara ya mbunge wa jimbo la Geita mjini Costantine Kanyasu alipotembelea katika shule ya msingi ikulwa kukagua ujenzi wa matundu 17 ya vyoo unaoendelea katika eneo hilo.

Sauti za afisa elimu kata na diwani
Mbunge Kanyasu akikagua maendeleo ya ujenzi wa matundu ya vyoo. Picha na Edga Rwenduru

Changamoto ya maji katika kata hiyo haiathiri taasisi ya elimu pekee bali hata wananchi wa kawaida, Emiliana Katemi na  Butimanye Malagilo ni wakazi wa kijiji cha Nyakahengere ambao pia wanaeleza changamoto hiyo inavyoathiri maendeleo ya familia kutokana na kutembea umbali mrefu kutafuta maji

Sauti ya wananchi
Mbunge wa Geita mjini Constantine Kanyasu akizungumza na wananchi (hawapo pichai) baada ya kufanya ziara kata ya Ihanamilo. Picha na Edga Rwenduru

Mbunge wa jimbo la Geita Mjini Costantine Kanyasu anabainisha mikakati ya kutatua changamoto hiyo.

Sauti ya mbunge Kanyasu