Storm FM

Sakata la mgomo wafanyabiashara lafika Katoro Geita

27 June 2024, 2:21 pm

Baadhi ya maduka yakiwa yamefungwa katika mamlaka ya mji mdogo wa Katoro. Picha na Evance Mlyakado

Sakata la mgomo kwa wafanyabiasha lililoanzia soko la kariakoo jijini Dar es salaam limeendelea kuchukua sura mpya katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania.

Na: Evance Mlyakado – Geita

Wafanyabiashara wa Mamlaka ya mji mdogo wa Katoro mkoani Geita jana Juni 26, 2024 wameungana na wafanyabiashara wenzao kutoka katika mikoa mbalimbali kushiriki mgomokwa kile wanachokidai kuwepo kwa kodi kubwa ambazo ni kandamizi kwao

Wakizungumza na Storm FM wameonesha kuguswa na suala hilo na kuiomba serikali kuweka utaratibu mzuri ili kuondoa changamoto hiyo.

Yohana Kasumile mfanyabiashara katika soko la Katoro. Picha na Evance Mlyakado

Makamu mwenyekiti wa wafanyabiashara soko la Katoro Peter Sanga amesema mazingira magumu ya kibiashara hasa katika ulipaji wa kodi ndiyo chanzo kikuu cha mgomo huo huku akiongeza kuwa wafanyabiashara wa katoro wanafuata maelekezo kutoka kwa viongozi wao wa ngazi za juu kitaifa.

Sauti ya makamu mwenyekiti
Makamu mwenyekiti wa wafanyabiashara soko la Katoro Peter Sanga. Picha na Evance Mlyakado

Mchambuzi na wa masuala ya uchumi kutoka jijini Dar es salaam, Dkt. Lenny Kasoga amesema kinachoendelea hivi sasa ni mwamko mpya kiuchumi uliopo miongoni mwa watanzania huku akiongeza kuwa kupuuzwa na kutokufanyiwa kazi kwa malalamiko ya wafanyabiashara wa Kariakoo hapo awali ndio kumepelekea kuibuka kwa hali hii.

Sauti ya mchambuzi wa uchumi