Storm FM

NELICO yatoa vitimwendo 50 kwa watoto wenye ulemavu Geita

18 June 2024, 7:41 pm

Mkuu wa wilaya ya Geita wa pili kulia akipokea vitimwendo 50 kutoka shirika la NELICO Geita. Picha na Mrisho Sadick

Katika kupunguza changamoto kwa watoto wenye ulemavu mashirika mbalimbali mkoani Geita yameombwa kuendelea kujitokeza kulisaidia kundi hilo.

Na Mrisho Sadick – Geita

Shirika la NELICO Mkoani Geita limeadhimisha siku ya mtoto wa afrika kwa kutoa viti mwendo 50 na bima za afya 50 kwa watoto wenye ulemavu ili kuwaondolea changamoto ya kutoka sehemu moja kwenda nyingine.

Mkurugenzi mtendaji wa shirika hilo mkoani Geita Paulina Alex akiwa katika maadhimisho hayo leo Juni 18,2024 ambayo kimkoa yamefanyika katika kata ya Nyamigota wilayani Geita Mkoani Geita amesema viti hivyo vimegharimu fedha zaidi ya milioni 15.

Mkuu wa wilaya ya Geita akikabidhi bima ya afya kwa mtoto mwenye ulemavu Geita. Picha na Mrisho Sadick

Sambamba na hayo Majogoro amesema katika kuadhimisha siku ya mtoto wa afrika shirika hilo litatumia milioni 25 kusasaidia kurudisha tabasamu kwa watoto 50 waliozaliwa na tatizo la mdomo sungura nakwamba kila mtoto atagharimu shilingi laki tano (500,000).

Sauti ya Mkurugenzi NELICO
Mkuu wa wilaya ya Geita akiwa na matoto mwenye ulemavu baada ya kukabidhiwa kitimwendo. Picha na Mrisho Sadick

Akizungumza kwaniaba ya mkuu wa mkoa wa Geita mkuu wa wilaya ya Geita Hashim Komba amelipongeza shirika la NELICO kwa kuendelea kuisaidia serikali kupunguza changamoto kwa watoto wenye ulemavu nakuyataka mashirika mengine mkoani Geita kuiga mfano huo kwa maslahi mapana ya taifa.