Storm FM

Mgogoro wa ardhi chanzo ujenzi wa kanisa kusimama Geita

29 May 2024, 1:59 pm

Baadhi ya viongozi na wananchi wakiwa katika eneo ambalo ujenzi umesimama. Picha na Kale Chongela

Migogoro ya ardhi hutajwa kupelekea changamoto mbalimbali ikiwemo kuvunjwa majengo, ujenzi kusimama na wakati mwingine watu hufikishana mahakamani ili kupata suluhu.

Na: Kale Chongela – Geita

Ujenzi uliokuwa ukiendelea wa kanisa la Pentekoste  FPCT mtaa wa Mbugani  kata ya Kalangalala mjini Geita umesimama kutokana na eneo hilo kuwa na mgogoro kati ya kanisa na shule.

Maamuzi hayo yamefanyika mara baada  ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi wilaya ya Geita Bw. Robert Nyamaigolo kufika eneo hilo kufutia malalamiko ya muda mrefu ya wananchi wa eneo hilo juu ya eneo la shule kuporwa na kuanziswa ujenzi wa kanisa.

Sauti ya mwenyekiti jumuiya ya wazazi

Askofu wa kanisa la FPCT mtaa wa Mbungani mchungaji Devid Nzumbi amesikitishwa na kitendo kilichofanyika cha ujenzi kusitishwa ili hali yeye anazo hati miliki za eneo hilo.

Sauti ya mchungaji FPCT

Afisa ardhi kutoka halmashauri ya mji wa Geita Bw. Mwizarubi Selestine amesimamisha ujenzi huo kufutia kuwepo kwa mgogoro hadi hapo mwafaka utakapopatikana.

Sauti ya afisa ardhi

Katibu wa malezi na mazingira jumuiya ya wazazi wilaya ya Geita Bw. Mapungo Paschal ametumia fursa hiyo kuwasihi afisa ardhi kujikita kutatua migogoro inayotokana na mipaka ya viwanja.

Sauti ya katibu