Storm FM
Storm FM
24 December 2025, 7:16 pm

Kuelekea sikukuu za mwisho wa mwaka, Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita atoa wito kwa wananchi kuendelea kudumisha amani na utulivu wakati wa kusheherekea.
Na: Ester Mabula
Kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Geita SACP Safia Jongo ametoa rai kwa wananchi wa mkoa wa Geita kusheherekea sikukuu za mwisho wa mwaka kwa amani na utulivu huku akiwasihi wazazi na walezi kuwalinda watoto wao.
Ametoa rai hiyo leo Disemba 24, 2025 akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake na kusema Jeshi la polisi mkoa wa Geita limejpanga vyema kuimarisha hali ya ulinzi na usalama katika maeneo yote ya mkoa.

Aidha amewasihi wazazi na walezi kuwa makini na watoto wao katika kipindi hiki ili kuondoa changamoto za ukatili zinazoweza kuwapata watoto.
Katika hatrua nyingine amewakumbusha watumiaji wa vyombo vya moto hususani madereva kuwa makini wakati wanapotumia barabara ili kuepusha ajali za barabarani,
