Storm FM

Nondo za Reuben Sagayika akiomba kura za CCM Msufini

6 October 2025, 7:41 pm

Mgombea udiwani kata ya Kalangalala (CCM) Reuben Sagayika akizungumza na wananchi wa Msufini (hawapo pichani). Picha na Ester Mabula

“Ninaimani kata ya Kalangalala itakwenda kubadilika kimaendeleo iwapo mtanipa kura za NDIO ili niweze kuwatumikia kwa moyo wangu” – Reuben Sagayika

Na: Ester Mabula

Mgombea udiwani wa kata ya Kalangalala kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Reuben Sagayika leo Oktoba 06, 2025 ameendeleza kampeni za kunadi sera zake na ilani ya CCM ambapo amezungumza na wakazi wa eneo la Msufini kata ya Kalangalala, halmashauri ya manispaa ya Geita.

Katika mkutano huo Sagayika amewaomba wakazi wa kata ya Kalangalala na wananchi kwa ujumla kuchagua viongozi watokanao na CCM katika ngazi za Udiwani, Ubunge na Urais ili kuleta maendeleo kwa Jamii.

Wakazi wa eneo la Msufini waliojitokeza kusikiliza sera za mgombea udiwani. Picha na Ester Mabula

Akizungumza mbele ya Mgombea Ubunge wa jimbo la Geita mjini Mhandisi Chacha Wambura ametoa maombi matatu ambayo ataanza nayo katika utatuzi wa changamoto iwapo atapata ridhaa ya kuchaguliwa kwa kuzingatia makundi ya vijana, wanawake pamoja na wazee.

Sauti ya mgombea udiwani kata ya Kalangalala Reuben Sagayika
Wakazi wa eneo la Msufini waliojitokeza kusikiliza sera za mgombea udiwani. Picha na Ester Mabula