Storm FM

TAKUKURU Geita yawafunda wasimamizi wa uchaguzi

12 September 2025, 4:34 am

Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Geita James Ruge akizungumza na washiriki. Picha na Edga Rwenduru

Tanzania inajiandaa na Uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025 ambapo rai imetolewa kwa wasimamizi wa uchaguzi kuepuka vitendo vya Rushwa.

Na: Edga Rwenduru

Taasisi ya kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Geita imewaonya wananchi na wasimamizi wa uchaguzi watakaobainika kugushi nyaraka za uchaguzi kwa lengo la kuwatafutia ushindi baadhi ya wagombea.

Akizungumza Septemba 11, 2025 wakati wa mafunzo yaliyoandaliwa na TAKUKURU kwa wasimamizi wa uchaguzi mkoa wa Geita, Kamanda wa TAKUKURU wilaya ya Geita Said Lipunjaje ambaye alikuwa ni mwezeshaji mada katika warsha hiyo amesema TAKUKURU wapo makini kufatilia wasimamizi ambao watakiuka maadili.

Sauti ya kamanda wa TAKUKURU Said Lipunjaje

Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Geita James Ruge amesema Taasisi hiyo inalenga kufikisha elimu ya mapambano dhidi ya Rushwa kwa wananchi katika kipindi hiki cha uchaguzi.

Sauti ya mkuu wa TAKUKURU Geita James Ruge
Baadhi ya washiriki wa warsha iliyoandaliwa na TAKUKURU mkoa wa Geita. Picha na Edga Rwenduru

Nao baadhi ya wasimamizi wa uchaguzi walioshiriki katika warsha hiyo wamesema wapo tayari kutekeleza maelekezo yote waliyopewa na TAKUKURU ili kuhakikisha uchaguzi unakuwa wa huru na haki.

Sauti ya wasimamizi wa uchaguzi
Baadhi ya washiriki wa warsha iliyoandaliwa na TAKUKURU mkoa wa Geita. Picha na Edga Rwenduru