Storm FM

Wananchi Nyantorotoro B waomba alama za barabarani

18 March 2025, 2:49 pm

Muonekano wa barabara eneo la Ubaoni, Nyantorotoro B. Picha na Kale Chongela

Alama za barabarani hutajwa kusaidia katika muongozo wa matumizi ya barabara sambamba na kurahisisha watumiaji kuepukana na ajali za barabarani.

Na: Kale Chongela – Geita

Wananchi wa mtaa wa Nyantorotoro B eneo la Uboani, kata ya Nyankumbu, halmashauri ya manispaa ya Geita wamedai kukabiliwa na changamoto ya ukosefu wa alama za barabarani katika eneo hilo jambo ambalo linawapa wakati mgumu wakati wa kuvuka.

Wakizungumza  na Storm Fm Marchi 17, 2025 baadhi ya wananchi wa eneo hilo wameeleza kuwa kutokuwepo kwa alama ya watembea kwa miguu inasababisha baadhi ya wananchi kuvuka eneo hilo kwa wasiwasi huku wakiomba serikali kutatua changamoto hiyo.

Sauti ya wananchi

Mkuu wa kitengo cha matengenezo kutoka ofisi ya Meneja wa TANROADS mkoa wa Geita Mhandisi Fredrick Mande amekiri kuwepo kwa ukosefu wa alama hizo za wavuka kwa miguu na kueleza kuwa  bado matengenezo yanaendelea kufanyika katika barabara hiyo kwani mkandarasi anayetekeleza uboreshaji wa lami bado hajakamilisha.

Sauti ya Meneja TANROADS Fredrick Mande