Storm FM

Mwenyekiti akemea mabalozi kuomba wananchi fedha ya utambulisho

17 February 2025, 2:49 pm

Baadhi ya wananchi mtaa wa Mwatulole wakiwa katika mkutano. Picha na Kale Chongela

“Wananchi wengi wanaogopa kujitambulisha kwa balozi sababu ya kuombwa elfu tano jambo ambalo halikubaliki katika mtaa wangu” – Mwenyekiti

Na: Kale Chongela – Geita

Serikali ya mtaa wa Mwatulole kata ya Buhalahala halmashauri ya manispaa ya Geita imewataka mabalozi wa mashina katika mtaa huo kutowatoza  wananchi shilingi 5000 kama kiingilio kwenye mtaa huo.

Rai hiyo imetolewa na mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Mwatulole Edward Msalaba akiwa kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Februari 17, 2025 katika ukanda wa Samandito ambapo amesema changamoto ya baadhi ya wananchi kushindwa kwenda kujitambulisha kwa mabalozi ni kutokana na baadhi ya mabalozi  kuwaomba fedha wananchi.

Sauti ya mwenyekiti Edward Msalaba

Kwa upande wake Balozi wa Shina 6, Benjamin Philibert amekanusha taarifa hizo kwenye mkutano wa hadhara kuwa yeye hajawahi kumtoza mwananchi kiasi chochote cha fedha kama sehemu ya kiingilio.

Sauti ya balozi Benjamin Philibert

Baadhi ya wananchi  walioshiriki Mkutano huo wa hadhara uliokutanisha  wananchi kutoka katika Balozi  3 shina 02,shina 03 na shina 06 wamesema endapo kila balozi atasimamia majukumu yake itampa wepesi mwananchi kwenda kujitambulisha kwa balozi  pindi anapohamia katika eneo lake.

Baadhi ya wananchi wakiwa katika mkutano wa hadhara. Picha na Kale Chongela