Storm FM

Achapwa viboko kwa tuhuma za kuiba kuni Msalala road

6 February 2025, 4:00 pm

Kijana aliyechapwa viboko na wananchi kwa tuhuma kuiba kuni. Picha na Amon Mwakalobo

“Wezi wametuchosha tutaendelea kuwatandika viboko ili waache kutuibia mali zetu” – Mwananchi

Na: Amon Mwakalobo – Geita

Mwananume mmoja mwenye umri wa miaka 36 aliyejitambulisha kwa jina moja la  Omary mkazi wa mtaa wa Mission halmashuri ya manispaa ya Geita ameambulia kichapo kutoka kwa  wananchi wenye hasira kutoka  mtaa wa Msalala road baada ya kukutwa akiiba kuni kwa mwanamke mmoja mkazi wa mtaa huo.

Akizungumza na Storm FM mmiliki wa kuni hizo amesema aliambiwa na jirani yake aliyemuona akiiba na ndipo akamkamata na kumpeleka ofisi ya Setikali ya Mtaa, huku akisema amekuwa akiibiwa kuni zake mara kwa mara.

Sauti ya mmiliki wa kuni

Mtuhumiwa Omary amesema ni mara ya kwanza kuiba kuni hizo hivyo akaomba msamaha huku akiahidi kutorudia tena kuiba.

Sauti ya mtuhumiwa

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo amesema wamechoshwa na tabia za wezi katika mtaa huo,na kuwaonya wezi waache tabia hiyo.

Sauti ya shuhuda

Kamanda mkuu wa sungusungu mtaa wa Msalala road Tumaini Lucas akizungumza kwa niaba ya mwenyekiti wa serikali ya mtaa huo, amewaonya wanaofanya matukio ya wizi mtaani hapo kuacha mara moja na endapo wataendelea wakiwakamata wataendelea kuwashughulikia.

Sauti ya kamanda wa sungusungu