

1 February 2025, 1:26 pm
Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa mkoani Geita kwa mwezi Oktoba hadi Disemba mwaka 2024 imepokea jumla malalamiko 43, makosa ya rushwa yakiwa ni 32 na yasiyohusu rushwa yakiwa 11.
Na: Daniel Magwina – Geita
Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Geita Azza Mtaita ameeleza hayo Januari 31, 2025 wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake juu ya mwenendo wa makosa mbalimbali.
Mtaita amesema idara zilizo lalamikiwa na wananchi ni serikali za mitaa malalamiko 7,elimu 4,utawala 5, afya 6,mahakama 2, fedha 2,nishati 2,ujenzi 4,sekta binafsi 1,vyama vya ushirika 2,ardhi 1,manunuzi 3,madini 1,mifugo 1,usafirishaji 1 na tasaf 1.
Mkuu wa TAKUKURU ameongeza kuwa malalamiko 32 uchunguzi wa awali umeshawasilishwa na malalamiko 11 walalamikaji wake wameeimishwa na kupewa ushauri.