Storm FM

GGML kuendelea kufadhili miradi kupitia CSR

14 October 2024, 11:54 am

Makamu wa Rais mwandamizi wa Anglo Gold Ashanti Afrika Terry Strong akihutubia katika kilele cha maonesho ya teknolojia ya madini Geita.

Mkoa wa Geita umeendelea kujivua uwepo wa mgodi wa GGML kwa kuwa umekuwa chachu ya maendeleo kwa wananchi katika nyanja mbalimbali hususani katika sekta za elimu na afya.

Na: Ester Mabula – Geita

Mgodi wa GGML umeahidi kuendelea kushirikiana na serikali katika nyanja mbalimbali za kiuchumi ikiwemo kutekeleza miradi ya maendelea kupitia sera ya uwajibikaji wa makampuni kwa jamii (CSR).

Akizungumza mbele ya Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Oktoba 13, 2024 katika hafla ya ufungaji wa maonesho ya saba ya kitaifa ya teknolojia na uwekezaji katika sekta ya madini makamu wa Rais mwandamizi wa Anglo Gold Ashant Afrika Terry Strong amesema Kupitia CSR, GGML inatenga zaidi ya shilingi Bilioni 9 kila mwaka kwaajili ya kuwekeza katika elimu, afya, miundombinu, namiradi ya kuongeza kipato ili kuboresha maisha.

Sauti ya Terry Strong

“Kulingana na ripoti ya TEITI ya hivi karibuni, GGML ilichangia asilimia 31.7 ya michango yote ya CSR kwenye sekta ya madini, na kuufanya mgodi huo kuwa mchangiaji mkubwa zaidi wa CSR.

GGML imejikita katika kuunda ajira, kujenga ujuzi, na kuinua uchumi wa ndani na kwamba kwa sasa wana ajira zaidi ya watu 6,900 wakiwemo wakandarasi, ambapo asilimia 98 ni Watanzania na zaidi ya asilimia 80 wakiwa katika nafasi za uongozi wa juu” – amesema Terry Strong.

Viongozi na wafanyakazi wa GGML wakiwa katika banda lao kwenye maonesho ya madini ambayo yamehitishwa katika uwanja wa EPZA.

Rais Samia amesema serikali itaendelea kuwekeza kwa wachimbaji wadogo na kwamba wamenunua mitambo 15 ya kuchoronga miamba kwa ajili ya wachimbaji wadogo.

Sauti ya Rais
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan wakati wa kilele cha maonesho ya madini Geita.

Mkuu wa mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela ameomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kubadilisha jina la uwanja wa maonesho ya EPZA na kuuita “Uwanja wa maonesho wa Samia.”

Sauti ya RC Geita