Storm FM

Ujenzi wa ofisi ya CCM kata ya Buhalahala waanza

28 September 2024, 9:46 am

Zoezi la ukataji utepe kuashiria kuanza kwa shughuli za uchimbaji msingi kwaajili ya ujenzi wa ofisi ya CCM kata ya Buhalahala. Picha na Edga Rwenduru

Wana-CCM kata ya Buhalahala wameanza mchakato wa ujenzi wa ofisi ya chama hicho katika kata hiyo ili kuondoa changamoto ya muda mrefu ya kukosa ofisi.

Na: Edga Rwenduru – Geita

Wanachama wa chama cha mapinduzi CCM kata ya Buhalahala iliyopo wilayani Geita wameshiriki kwa pamoja  katika uchimbaji wa msingi kwaajili ya ujenzi wa ofisi ya chama hicho inayojengwa katika mtaa wa mwatulole.

Mwanachama wa CCM kata ya Buhalahala akishiriki zoezi la uchimbaji wa msingi kwaajili ya ujenzi wa ofisi ya chama. Picha na Edga Rwenduru

Wakizungumza na Storm Fm wanachama hao wamesema endapo ujenzi wa ofisi hiyo utakamilika utaenda kutatua changamoto ya wanachama kupata huduma kwa urahisi kwani hata mikutano ya chama ilikuwa wanalazimika kuifanyia chini ya miti.

Sauti ya wanachama

Mwenyekiti wa Chama hicho kata ya Buhalahala Mwisa Elias Kabese pamoja na John Mwanda ambaye ni mtaalamu anayesimamia ujenzi wa ofisi hiyo wamesema ujenzi wa ofisi utagharimu zaidi ya milioni 90 na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba mwaka huu.

Sauti ya mwenyekiti na fundi
Mwenezi wa CCM wilaya ya Geita Gabriel Nyansilu akiendelea na zoezi la uchimbaji msingi. Picha na Edga Rwenduru

Naye Mwenezi wa chama cha mapinduzi CCM Wilaya ya Geita Gabriel Nyansilu ambaye alikuwa mgeni rasimi katika uzinduzi wa ujenzi huo pamoja na Manjale Magambo mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Geita wamewataka wananchama wa chama hicho kata ya Buhalahala kuzidisha ushirikiano.

Sauti ya Mwenezi na Mwenyekiti UVCCM