Storm FM

Maulid kitaifa kufanyika mkoani Geita

6 September 2024, 7:53 am

Sheikh wa mkoa wa Geita Alhaj Yusuph Kabaju akizungumza na waandishi wa habari mkoani Geita. Picha na Kale Chongela

Sherehe za Maulid ni maadhimisho ya kuzaliwa kwa Mtume uhammad (SAW) ambayo huadhimishwa kila mwaka katika mwezi wa Rabiul Awwal kwenye kalenda ya kiislamu ambapo siku hii ilianza rasmi kusheherekewa katika karne ya 12.

Na: Kale Chongela – Geita

Baraza la waislamu Tanzania BAKWATA mkoa wa Geita wanatarajia kufanya sherehe za Maulid kitaifa mkoani Geita katika viwanja vya CCM Kalangalala mjini Geita.

Akizungumza na waandishi wa habari septemba 05, 2024 Sheikh wa mkoa wa Geita Alhaj Yusuph Kabaju amesema sherehe hizo zitafanyika Septemba 15-16, mwaka huu ambapo mkoa wa umepewa heshima kubwa ya kuandaa sherehe hiyo ambapo wageni mbalimbali watakuwepo akiwemo Sheikh mkuu wa Tanzania Muft Abubakar Zuber Bin Ally Mbwana.

Sauti ya sheikh wa mkoa
Muonekano wa nje wa msikiti mkuu wa Ijumaa ulipo katika halmashauri ya mji wa Geita. Picha na Kale Chongela

Katibu wa baraza kuu la waislamu Tanzania BAKWATA mkoa wa Geita Abas Mtuguja amebainisha kuwa sherehe hiyo itaambatana na uwepo wa maonesho ya wajasiriamali katika uwanja wa CCM Kalangalala ambayo yataanza Septemba 07, 2024.

Sauti ya katibu