Storm FM

Watu wanne wakamatwa na mali za wizi Geita

25 June 2024, 1:12 pm

Kamanda wa polisi mkoa wa Geita SACP Safia Jongo akionesha baadhi ya mali za wizi kwa waandishi wa habari (hawapo pichani). Picha na Evance Mlyakado

Licha ya jitihada za Jeshi la polisi mkoani Geita kuendelea kuimarisha ulinzi, bado vitendo vya wizi na uporaji vinaendelea kujitokeza katika baadhi ya maeneo mkoani Geita.

Na: Evance Mlyakado – Geita

Watu wanne akiwemo Ezekieli Misalaba maarufu kama ‘Mr. Masamaki” mkazi wa Nyankumbu wanashikiliwa na Jeshi a polisi mkoani Geita kwa tuhuma za kujihusisha na matukio ya wizi katika mitaa mbalimbali mjini Geita.

Kamanda wa polisi Geita SACP Safia Jongo akkitoa taarifa ya matukio ya uharifu kwa vyombo vya habari

Watuhumiwa hao wakiwa katika maeneo mbalimbali ya mji wa Geita wametiwa nguvuni na jeshi la polisi katika operesheni iliyofanyika Juni 22, 2024 ambapo katika operesheni hiyo zaidi ya baiskeli 30, magodoro, redio na vitu vingine mbalimbali vimekamatwa.

Baiskeli zilizopatikana katika operesheni ya jeshi la polisi. Picha na Evance Mlyakado

Kamanda wa Jeshi la polisi mkoani Geita, Kamishina msaidizi mwandamizi wa jeshi la polisi (SACP) Safia Jongo amethibitisha kukamatwa kwa watuhumiwa hao na kubainisha hatua sitahiki zilizochukuliwa na jeshi hilo.

Sauti ya kamanda Jongo
Baadhi ya mali za wizi zilizopatikana katika operasheni. Picha na Evance Mlyakado

Awali katika mtaa wa Mwabasabi ambapo vitu vingi viliweza kukamatwa kwenye nyumba ya mmoja kati ya watuhumiwa hao wanne, wananchi na majirani wameonesha kushangazwa na tukio hilo kwani hawakutarajia kama jirani yao angekuwa akijihusisha na  vitendo vya wizi.

Baadhi ya wananchi na majirani wa mtuhumiwa wakishangaa mali za wizi kuonekana. Picha na Evance Mlyakado