Storm FM

GGML yakabidhi nyumba 6 na pikipiki 50 kwa jeshi la polisi Geita

7 October 2024, 10:10 am

Miongoni mwa nyumba 6 zilizokabidhiwa kwa Jeshi la polisi mkoani Geita. Picha na Evance Mlyakado

Mgodi wa Geita Gold Minning Limited umekabidhi nyumba 6 na pikipiki 50 kwa Jeshi la polisi mkoani Geita ikiwa ni sehemu ya urejeshaji wa Jamii (CSR).

Na: Evance Mlyakado – Geita

Naibu waziri mkuu na waziri wa nishati Dkt. Doto Mashaka Biteko Oktoba 05, 2024 amezindua nyumba sita zenye thamani ya shilingi bilioni 1.8 zilizojengwa na mgodi wa uchimbaji madini ya dhahabu wa GGML kwaajili ya makazi ya maafisa wa Jeshi la polisi.

Kamanda wa polisi mkoa wa Geita SACP Safia Jongo akisoma taarifa ya mradi wa nyumba za polisi. Picha na Evance Mlyakado.

Awali akitoa taarifa ya ujenzi wa mradi huo kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Geita SACP Safia Jongo ameeleza tathmini na taarifa ya utekelezaji wa mradi huo

Sauti ya RPC Jongo

Makamu wa Raisi wa Anglo Gold Ashanti Afrika, Simon Shayo amesema nyumba hizo zilizopo katika mtaa wa Magogo kata ya Bombambili wilayani Geita ni sehemu ya Urejeshaji wa GGML Kwa Jamii (CSR)

Sauti ya Simon Shayo
Makamu wa Rais wa Anglo Gold Ashanti Afrika Simon Shayo akizungumzia mradi wa nyumba zilizokabidhiwa. Picha na Evance Mlyakado

Naibu waziri mkuu na waziri wa Nishati Doto Mashaka Biteko ambaye alikuwa mgeni rasmi ameipongeza wizara ya madini kwa usimamizi mzuri wa sheria mbalimbali za madini ambazo zimesaidia Kwa kiasi kikubwa kuchochea ukuaji wa maendeleo katika maeneo mbalimbali.

Sauti ya naibu waziri
Naibu waziri mkuu na waziri wa nishati Dkt. Dotto Biteko akizindua nyumba za polisi zilizofadhiliwa na GGML