Nuru FM

Milioni 407.9 yatolewa kwa vikundi 71 iringa

12 December 2025, 12:05

Mfano wa Hundi ya Shilingi Milion 407.9 inayotolewa kwa vikundi 71. Picha na Hafidh Ally

“Fedha hizi zitumike kwenye kuleta maendeleo ambayo mmeyaandikia kwenye miradi yenu”

Na Hafidh Ally

Jumla ya vikundi 71 vinavyoundwa na wananchi wanaojishughulisha na kilimo, ufugaji na viwanda vidogo katika Halmashauri ya wilaya ya Iringa wamepata mikopo ya Asilimia 10 yenye thamani ya Shilingi Milioni 407.9.

Mkuu wa Idaya ya Maendeleo Wilaya ya Iringa Saumu Mweka amesema kuwa Mikopo hiyo imetolewa kama sehemu ya mkakati wa Serikali kuwajengea uwezo wa kiuchimi wananchi na kuongeza ushiriki wao kwenye shughuli za uzalishaji mali hususani vijana, wanawake na wenye ulemavu na ikitarajiwa kuchochea ongezeko la uzalishaji, kukuza ajira na kuinua vipato vya wanufaika.

Sauti ya Saumu

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Iringa Benjamini Sitta amesema kuwa fedha zilizokabidhiwa kwa vikundi hivyo zinapaswa kupelekwa kwa kwenye miradi iliyokusudiwa.

Sauti ya DC

Kwa Upande wake Mwenyekiti Wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Steven Mhapa amewataka wananchi kutokopa fedha za Halmashauri kama huna shughuli za Kufanya ambapo mkopo huo siyo wa riba.

Sauti ya Mhapa

Mikopo hiyo inatarajiwa kuchochea ongezeko la uzalishaji, kukuza ajira na kuinua vipato vya wanufaika katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri hiyo hasa yale yaliyopo pembezoni.