Nuru FM

Mikopo umiza yatajwa kuvunja ndoa Mafinga

23 April 2026, 08:49

Diwani wa Kata ya Boma Baraka kisakanike akizungumzia kuhusu mikopo umiza. Picha na Fredrick Siwale

Mikopo ya Kausha Damu imepelekea wanawake kukimbia ndoa zao

Na Fredrick Siwale

Wananchi Halmashauri ya Mji wa Mafinga wamelalamikia kitendo vya taasisi zinazotoa mikopo kuwafuata na kuwafanyia fujo pale wanapofuata marejesho jambo linalowavunjia utu huku wengine wakiiishi kama wakimbizi.

Wakizungumza na nuru fm baadhi ya wananchi hao wamesema kuwa licha ya wao kukopa fedha katika taasisi hizo kwa maelewano, bado maafisa wa taasisi hizo wanashindwa kuwadai kwa staha huku wakifika nyakati za usiku kuwatafuta wadaiwa.

Sauti ya Wananchi

Aidha wanachi hao wameiomba serikali kuingilia kati kwa kuziiita Taasisi zilizowakopesha fedha ili wajue namna ya kulipa kwani jambo hilo limepelekea baadhi ya wanawake kukimbia ndoa zao.

Sauti ya Wananchi

Naye Mwenyekiti  wa Serikali ya mtaa wa Ivambinungu Uliopo Halmashauri ya Mji Mafinga Bw. Isaack Kikawa amesema kuwa ni kweli wanawake wamekuwa wakikopa fedha Bila kuwashirikisha waume zao jambo lililopeleka ndoa kuvunjika.

Sauti 3 Mwenyekiti

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Boma Baraka kisakanike amezitaka taasisi zinazokopesha fedha kutumia kfuata haki za msingi pale wanapofuata marejesho yao na kuacha kuwadhalilisha wakopaji.

Sauti 4 Diwani