Nuru FM

DC Kheri: TRAMPA tunzeni siri za serikali

8 May 2024, 12:33 pm

Mkuu wa wilaya ya Iringa Kheri James  akizungumza na Wana TRAMPA Mkoani Iringa. Picha na Adelphina Kutika

Watunza kumbukumbu za Mamlaka za Serikali wametakiwa kudhibiti uvujishaji wa siri na nyaraka za serikali wanapotekeleza majukumu yao.

Na Adelphina Kutika

Wanataaluma wa Chama cha Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka Tanzania (TRAMPA) wametakiwa kuzingatia miiko ya taaluma yao hususan utunzaji siri za Serikali na kufuata utaratibu rasmi wa utoaji taarifa.

Agizo hilo amelitoa Mkuu wa wilaya ya Iringa ,Kheri James  kwa niaba ya Mkuu wa mkoa ,wakati akifungua mafunzo na kikao kazi maalumu kwa Wanataaluma wa Chama cha Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka Tanzania (TRAMPA) kutoka Tanzania bara na Visiwani yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano  wa Masiti Mkoani Iringa  ambapo amewahimiza  kuwa waaminifu mahala pa kazi.

Sauti ya DC Kheri

Awali, Mwenyekiti wa TRAMPA, Devotha Mrope akiwasilisha risala mbele ya mgni rasmI  ametumia fursa hiyo kueleza lengo la mafunzo hayo ni pamoja na kuwajngea uwezo na kuongeza tija na ufanisi katika utendaji kazi wao.

Sauti ya Mwenyekiti Trampa

Kwa upande wao baadhi ya washiriki  wa mafunzo hayo bi Dorkasi Brown na Atha Jonathan Kasongo wamelezea suala la utunzaji wa siri limekuwa ni changamoto kwa baadhi ya wanataaluma hao hivyo kupitia mafunzo hayo ni yatasaidia kudhibiti mianya hiyo.

Sauti ya washiriki

MWISHO