Nuru FM

Tembo wavamia mashamba Ruaha Mbuyuni

23 March 2024, 10:56 am

Tembo wakiwa katika mashamba ya wakulima. Picha na mwandishi wetu

Uwepo wa tembo katika kijiji cha Mtandika umetajwa kuwa kero kwani wamewasababishia hasara ya kuharibu mazao yao.

Na Adelphina Kutika.

WAKAZI wa Kijiji cha Mtandika kata ya Ruaha Mbuyuni wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa wameiomba serikali kuwaondoa Tembo wanaovamia mashamba yao na kusababisha hasara lakini pia kuhatarisha maisha yao kutokana na tembo hao kupita katika makazi yao.

Wakizungumza  katika mashamba hayo wananchi hao wamesema kuwa  Tembo hao mara kadhaa wamekuwa wakifika majira ya usiku na kuharibu mazao hasa zao la Mahindi na kuwapelekea kushindwa kurejesha mikopo waliyokopa kwenye mashirika ya kilimo.

Sauti ya wanakijiji wa Mtandandika

Aidha wameiomba viongozi wa serikali  kuwa na utaratibu wa kuwatembelea katika kijiji hicho ili kubaini changamoto zinazowakabili  husasani uvamizi wa tembo hao.

Sauti ya wanakijiji wa Mtandandika

Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji cha mtandika ADAMU ALLY MAKUNGA amesema amefanya jitihada za kuwasiliana na (TANAPA )  ili kufukuza  wanyama hao lakini hakuna mabadiliko yoyote katika kijiji hicho.

MWISHO