Nuru FM

Idydc Microcredit yawa Mkombozi kwa wajasiriamali Ifunda

15 May 2026, 15:08

Mnufaika wa Mkopo kutoka IDYDC Microcredit Bw. Hazil akizungumzia kuhusu mkopo ulivyomnufaisha kiuchumi. Picha na Hafidh Ally

“Mkopo kutoka IDYDC umesaidia kusomesha watoto na kukuza Biashara”

Na Hafidh Ally

Wananchi wa Kijiji cha Ifunda Wilaya ya Iringa wameishukuru Taasisi ya Utoaji Mikopo ya IDYDC Microcredit kwa kuwapatia Mikopo iliyowasaidia kuanzisha biashara na kujikwamua kiuchumi.

Wakizungumza na Nuru FM baadhi ya wananchi wa Kijiji hicho wamesema kuwa IDYDC imekuwa Mkombozi kwao, licha ya kukuza biashara zao, pia mikopo hiyo imewasaidia kusomesha watoto wao.

Sauti ya Wanufaika Ifunda

Aidha wananchi hao wamesema kuwa wamenufaika kwa kujikita katika kilimo huku wengine wakikiri kurudi kukopa kwa mara nyingine baada ya kuona manufaa waliyoyapata.

Sauti ya Wanufaika Ifunda

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Taasisi ya Utoaji Mikopo ya IDYDC Kanda ya Ifunda Joackim Kisinini amesema kuwa wananchi wa Kanda hiyo wamenufaika kwani kabla ya kukopa wanawapa elimu ya namna ya kufanya biashara.

Sauti ya Kisinini

Naye Meneja wa IDYDC Microcredit Anisia Mwinuka amesema kuwa wameweka kiwango kwa wale wanaokopa kwa mara ya kwanza mkopo usiozidi laki tano sambamba na kuwapatia semina ya biashara.

Sauti ya Bi. Mwinuka

IDYDC Microcredit ni Taasisi inayotoa mikopo kwa wajasiriamali wadogo na wakubwa ambayo iko katika eneo la Siasa ni Kilimo inalenga Kutoa huduma za kifedha zinazoweza kufikiwa kwa jamii ambazo hazijafikiwa vizuri nchini Tanzania ili kukuza uchumi na maendeleo endelevu.