Mazingira FM

Ufaulu, uripoti sekondari bado changamoto Bunda

3 February 2026, 6:23 am

Katibu Tawala wa Wilaya ya Bunda Salum Alfan Mtelela,picha na Catherine Msafiri

Katibu Tawala wa Wilaya ya Bunda Salum Alfan Mtelela, Ameeleza kuwa asilimia 30/31 mjini na asilimia 42 kwa vijijini wanafuzi hawakufaulu.akitoa wito wa kuhakikisha wanafunzi hao wanaripoti shuleni

Na Catherine Msafiri,

Katibu Tawala wa Wilaya ya Bunda Salum Alfan Mtelela, amesema kuwa licha ya wanafunzi kuhitimu mtihani wa kumaliza elimu ya msingi, kiwango cha ufaulu na uripoti shuleni bado hakiridhishi katika halmashauri zote za Mji wa Bunda na Wilaya ya Bunda.

Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya sheria, Mtelela amesema changamoto kubwa si ufaulu pekee bali pia ni idadi ndogo ya wanafunzi wanaoripoti kujiunga na elimu ya sekondari hata miongoni mwa waliofaulu mtihani wa darasa la saba.

Ameeleza kuwa asilimia 30/31 mjini na kwa vijijini ni asilimia 42 wanafuzi hawakufaulu.akitoa wito wa kuhakikisha wanafunzi hao wanaripoti shuleni

Sauti ya Katibu Tawala wa Wilaya ya Bunda, Salum Alfan Mtelela