Mazingira FM

Bima kwa chombo cha moto ni takwa la kisheria

2 April 2026, 17:51

ASP Buhembere: “Chanzo kikuu cha ajali ni matendo ya kibinadamu, mazingira na chombo chenyewe hivyo.”

Na Adelinus Banenwa

Wito umetolewa kwa wamiliki wote wa vyombo vya moto kuhakikisha wanakuwa na bima za vyombo hivyo ili kukidhi matakwa ya kisheria kama ilivyo ainishwa kwenye kifungu cha 168 cha sheria ya usalama barabarani na kifungu cha 169 cha sheria ya bima.

Hayo yamebainishwa leo na  Mrakibu msaidizi wa polisi ASP Faustin J. Buhembere na mkuu wa usalama barabarani wilaya ya Bunda kupitia kipindi cha asubuhi leo mazingira fm ambapo amesema chombo cha moto chenye bima hata kikipata ajali waathirika wanapata fidia kupitia bima hiyo.

ASP Buhembere ameongeza kuwa madereva kwa kiasi kikubwa ndiyo wanaowajibu kuhakiki chombo cha moto kabla ya kukitumia wanajiridhisha kuwa kina bima lakini na dereva mwenyewe awe na leseni.

ASP Buhembere amesema chanzo kikuu cha ajali ni matendo ya kibinadamu, mazingira na chombo chenyewe hivyo Pamoja na kuwa wanaweka na kusimamia sheria za usalama barabarani bado kuna watu wanavunja sheria hizo.

Sauti ya ASP Faustin J. Buhembere mkuu wa usalama barabarani wilaya ya Bunda

Kwa upande wake Halfan Isango Afisa ubora  kutoka mamlaka ya usimamizi wa Bima Tanzania TIRA kanda ya ziwa amesema wao kama TIRA wanasimamia wa bima wanasimamia masuala mbalimbali ikiwemo kutoa ithibati kwa mawakala wa  utoaji huduma za bima ikiwemo vyombo vya moto

Isango pia amesema jukumu linguine ni kutoa elimu kwa jamii na wamiliki na watumiaji vyombo vya moto kujua umuhimu wa vyombo hivyo pia kushughulikia malalamiko yote yanayohusu bima.

Sauti ya Halfan Isango Afisa ubora TIRA