Mazingira FM
Mazingira FM
31 January 2026, 12:12 pm

Katika msaada huu Benk ya NMB imetoa vifaa vyenye thamani ya shilingi milioni 230 mkoani Mara ambapo kwa hospital DDH Rorya imepokea Encubators 8 ambazo zitasaidia watoto njiti baada ya kuzaliwa.
Na Adelinus Banenwa
Imeelezwa kuwa ukosefu wa vifaa saidizi kwa watoto njiti ( Encubators) husababisha vifo kwa asilimia 40 wilayani Rorya ambapo katika hospital moja watoto 280 wanaozaliwa kwa mwezi watoto 30 kati yao huzaliwa chini ya umri.
Hayo yamesemwa na Dr Halfan Haule mkuu wa wilaya ya Rorya kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Mara Mhe Kanal Evans Mtambi katika hafla ya kupokea vifaa vya hospitali na shule kutoka Bank ya NMB
Dkt Halfani kwa niaba ya mkuu wa mkoa ameishukuru bank hiyo kwa msaada huo walioutoa kwa hospitali na shule ndani ya mkoa wa Mara huku akitoa wito kwa waliopokea vifaa kuhakikisha vinatumika kama malengo yaliyokusudiwa.

Akikabidhi msaada huo Mkurugenzi na Afisa mkuu wa fedha wa Bank ya NMB Juma Kimori amesema bank hiyo imeendelea kuiunga mkono serikali katika kusaidia sekta za elimu, afya pamoja na majanga.
Katika msaada huu Benk ya NMB imetoa vifaa vyenye thamani ya shilingi milioni 230 mkoani Mara ambapo kwa hospital DDH Rorya imepokea Encubators 8 ambazo zitasaidia watoto njiti baada ya kuzaliwa.
Kimori amesema tangu NMB ianzishwe hadi mwaka 2025 jumla ya shilingi bilion 23 zimetolewa na bank hiyo kurudisha shukrani kwa wananchi.

Kwa upande wake Dr Bwire Chirangi Mganga mkuu hospitali ya Menonite Shirati Rorya amesema uwepo wa vifaa hivyo utasaidia kwa kiwango kikubwa kuhudumia akina mama wanaojifungua watoto njiti katika eneo hilo.
Aidha ameiomba serikali kuiongezea hospitali hiyo watumishi kutokana na mahitaji yaliyopo akidai zaidi ya wauguzi 10 waliyokuwa wakitoa huduma hospitalini hapo wameondoka baada ya kuajiriwa na serikali.