Mazingira FM

Mikopo asilimia 10 ipo ombeni

31 March 2026, 15:24

Octavina Kiwone Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya jamiii halmashauri ya Bunda

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya jamiii halmashauri ya Bunda Bi Octavina Kiwone ameeleza kuhusu fursa ya mikopo ya asilimia 10  ambapo amewataka vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kujitokeza kwa wingi  kuunda vikundi imara  vitakavyowasaidia kupata fursa hiyo ili waweze kujikwamua kiuchumi na kuinua kipato chao.

Akielezea umuhimu wa waombaji mikopo kuwa katika vikundi Bi Octavina amebainisha kuwa mfumo huo huongeza uwajibikaji, mshikamano na urahisi wa usimamizi wa mikopo hivyo kuongeza uwezekano wa urahisi wa urejeshaji kwa wakati.

Sauti ya Octavina Kiwone Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya jamiii halmashauri ya Bunda

Bi Octavina ametoa elimu kuhusu sifa za waombaji wa mikopo kwa wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu.

Alisisitiza umuhimu wa vikundi kusajiliwa rasmi, kuwa na mpango wa biashara wenye tija, pamoja na kuzingatia nidhamu katika urejeshaji wa mikopo ili kuwezesha watu wengi zaidi kunufaika na fursa hiyo ya asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri

Sauti ya Octavina Kiwone Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya jamiii halmashauri ya Bunda