Mazingira FM
Mazingira FM
30 March 2026, 10:27

Zaidi ya asilimia 96 ya watoto wanojiandikisha kuanza shule za msingi na sekondari wote wanafika shuleni.
Na Mariam Mramba
Mkuu wa wilaya ya Bunda, Mhe Aswege Enock Kaminyoge amewapongeza wananchi wa kata ya Mgeta kwa kufanikisha kwa kiwamgo kikubwa uandikishaji na mahudhurio ya wanafunzi ambapo zaidi ya asilimia 96 ya watoto wanojiandikisha kuanza shule za msingi na sekondari wamehakikisha wanafika shuleni.
Hayo amesama hivi karibuni alipokuwa akizungumza na wananchi hao ambapo DC Kaminyoge amesema hatua hiyo ni ya kupongezwa kwani inaonesha uelewa mkubwa wa jamii kuhusu umuhimu wa elimu kwa maendeleo yawatoto na taifa kwa ujumla
Aidha mkuu huyo wa wilaya amewataka wananchi hao kuendelea kushirikiana kwa karibu kuhakikisha wanafunzi hao wanapata chakula shuleni ili kuwasaidia kuwa na afya njema, kuongeza umakini darasani na hatimaye kufanya vizuri katika masomo yao.

Kaminyoge ameainisha kuwa lishe bora ni msingi muhimu wa mafanikio ya kielemu na kuwahimiza wazazi kutekeleza jukumu hilo kikamilifu