Mazingira FM
Mazingira FM
27 June 2025, 9:50 am

“kikao hicho siyo kampeni badala yake ni kumshukuru kiongozi huyo kwa yale aliyoyafanya”
Na Adelinus Banenwa
Baraza la wazee wa chama cha mapinduzi kata ya Nyasura Halmashauri ya mji wa Bunda mkoani Mara wamemkabidhi fedha kiasi cha shilingi elfu hamsini aliyekuwa diwani wa kata hiyo Magigi Samweli Kiboko kwa ajili ya kuchukua fomu ya kuomba kugombea udiwani wa kata hiyo.

Hafla hiyo iliyofanyika leo June 26, 2025 katika ofisi za CCM Nyasura wamesema katika kipindi cha miaka mitano iliyopita kiongozi huyo alifanya kazi nzuri ambapo amefanikisha kupatikana miradi yenye thamani ya shilingi bilion 3 katika kipindi cha miaka 5
Kw upande wake aliyekuwa Diwani wa kata hiyo Magigi Samweli Kiboko amesema kwa sababu ya baraka za wazee hao atachukua fomu baada ya mchakato wa chama kuanza mnamo 28 June 2025

Akizungumza mwenyekiti wa baraza la wazee chama cha mapinduzi kata ya Nyasura LUGEMBE K LUGEMBE amesema kikao hicho siyo kampeni badala yake ni kumshukuru kiongozi huyo kwa yale aliyoyafanya.